Utambuzi wa Magonjwa ya Ng’ombe (new) I Mshindo Media.

 MAGONJWA YA NG’OMBE.

Sifa za mnyama mwenye afya
i. Mchangamfu wakati wote macho maang’avu huku mkia na masikio vikimsaidia
kufukuza inzi
ii. Kula na kucheua, kunywa maji vizuri kila siku
iii. Kuonyesha ushirikiano na kutembea pamoja kwenye kundi
iv. Kutembea vizuri
v. Anastuka na kukimbia anapostuliwa na mnyama hatari anapomkaribia kama vile
mbwa mwitu, fisi, chui, simba.
vi. Mwili wake una uwezo mkubwa wa kukibadili chakula anachokula kutoa mazao ya
kutosha kama vile maziwa.
vii. Anaonekana mwenye nguvu na kwa wale wanaoendelea kukuna wanaongezeka
uzito kwa muda mfupi
viii. Kwa mnyama anayekamuliwa mara kwa mara kupiga kelele za kumtafuta mtoto
wake,kiwele huwa kimejaa maziwa, chuchu huwa wakati mwingine zimetanuka
upande kwa ajili ya kujaa maziwa
ix. Ngozi ya mnyama husisimka mara kwa mara wadudu wapomtambaa
x. Kwa madume, huwa wana hamu ya kuwapanda majike wanaoingia kwenye joto.
Miili yao hujengeka vizuri. Pumbu hujengeka na kukaa vizuri kwenye nafasi yake
(yaani katikati ya miguu)
xi. Pua na midomo huwa na unyevu unyevu wakati wote.
xii. Ngozi kuwa na ulaini unaotakiwa na manyoya hung’aa.
xiii. Kwa kawaida unapo mkaribia mnyama endapo amekaa chini ni lazima atanyanyuka

Dalili za Mnyama anayeumwa
i. Hukosa hamu ya kula na kunywa maji
ii. Mwili kunyong’onyea na kuonekana mchovu
iii. Mnyama kutembea pole pole na kwa taabu na mara nyingi hujitega na wenzake
iv. Pua zake na midomo huonekana kukauka.
v. Kupunguka kwa kiwango cha uzalishaji kama vile maziwa. Kwa madume huduwaa
na kuinamisha shingo chini na kukosa hamu ya kuwapanda majike wanaoingia
kwenye joto.

Vyanzo vya magonjwa
Magonjwa mengi ya mifugo husambazwa na vijidudu ambao huingia kwenye mfumo wa
damu na kusababisha homa na baadae madhara makubwa. Mangonjwa mengi ya mifugo
husababishwa na vyanzo kutoka nje ya mwili wa mnyama mfano mazingira machafu
anayoishi mnyama, vitu vinavyopelekea vidonda (Vitu vyenye ncha kali) husababisha
vidonda ambapo vimelea vinaweza kukaa.Pia mnyama anaweza kupata ugonjwa kutokana
na hali za ndani ya mwili kama upungufu wa lishe, mfano: madini, na na magonjwa ya
kulithi.

Mfano wa wadudu hao ni;
 Vimelea (bacteria)
Mfano wa magonjwa yanayosababishwa na bacteria ni chambavu, Blackquarter, Kimeta,
Kifua kikuuu, brucellosis (ugonjwa wa kutupa mimba) na ugonjwa wa kiwele.Ng’ombe
dume huvimba mapumbu.
 Virusi (virus) Otatis
Mfano wa magonjwa yanayosababishwa na virusi ni kichaa cha mbwa (Rabies), Ugonjwa
wa midomo,miguu (foot and mouth disease) na Sotoka (Rinderpest)
 Protozoa
Magonjwa yanayo sababishwa na protozoa ni kama ndigana baridi, ndigana kali, ndigana
mkojo damu, ndigana maji moyo na nagana.

Angalizo:
Magonjwa yote ya Ndigana husambazwa na makupe, wakati ugonjwa wa nagana
husambazwa na ndorobo.

Lishe duni.
Upungufu wa viinilishe katika chakula cha mifugo husababisha madhara katika mwili kama
ifuatavyo;
i. Husababisha majike kutopata joto mapema
ii. Ndama kuzaliwa na viungo visivyo komaa
iii. Upungufu wa uzalishaji maziwa
iv. Kiwango cha uzalishaji kushuka

Vidonda/michubuko.
Kupitia vidonda au michubuko, wadudu wasababishao magomjwa huweza kuingia mwilini
kwa mnyama

Magonjwa ya kurithi

Kama mmoja wa wazazi ana ugonjwa wa kurithi basi kuna uwezekano mkubwa kwa

mmoja wa ndama watakaozaliwa kurithi ugonjwa huo. Magonjwa yanayoenezwa na kupe.

 Ndigana kali.

Dalili zake
i. Homa kali hadi nyuzi joto 42c
ii. Povu kutoka mdomoni na puani
iii. Kuhara choo kilichochanganyikana na kamasi na damu
iv. Tezi kuvimba sana na zenye joto
v. Kuacha kula
vi. Ukungu kwenye macho
vii. Kifo baada ya wiki moja hadi mbili

Tiba
Butalex, Parvexon, tiba iambatane na sindano moja ya kuondoa uvimbe kwenye mapafu
kama hali hiyo tayari imeshajitokeza. Tumia Multivitamin ili kuongeza hamu ya kula na
Raxis ili kuondoa maji kwenye mapafu.

Kinga/zuia
Zingatia uogeshaji sahihi na Chanjo ya ECF

Ndigana baridi (Anaplasmosis).

Dalili zake

i. Homa hadi nyuzi joto 42C
ii. Kukosa hamu ya chakula
iii. Choo kigumu na makamasi na harufu mbaya
iv. Kifo baada ya siku 8 hadi 10

Tiba
i. Antibiotic kama vile Oxytetracycline
ii. Imizol.

Kinga
Zingatia uogeshaji sahihi
Mkojo damu (Babesiosis) ugonjwa wa kukojoa damu.
 Dalili zake.
i. Mkojo kuwa na rangi ya damu isiyokolea zambarau
ii. Mkojo hutoka kidogo kidogo na kwa muda mrefu
iii. Homa hadi nyuzi joto 40C
iv. Kuacha kula
v. Choo kigumu au kuhara wakati mwingine
vi. Kifo baada ya wiki 1

Tiba
Berenil ikisaidiwa na antibiotics za sindano kama vile oxytetracycline (OTC) pia tumia
Multivitamin kuongeza hamu ya kula.

Kinga
Zingatia uogeshaji sahihi

Moyo kujaa maji (heart water).

Dalili zake
i. Kizunguzungu na kuanguka,
ii. Kifo baada ya siku 2

Tiba

Antibiotics za sindano kama vile oxytetracycline.
 Kumbuka tiba lazima ifanywe mapema
iwezekanavyo
Kinga/kuzuia
Zingatia uogeshaji sahihi

Share Now

Related posts