UFUGAJI WA NGURUWE NA FAIDA ZAKE (new) I Mshindo media

Utangulizi 
Nguruwe ni mnyama ambaye hutumika kama chakula / mbonga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara. 

NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFUATAYO 
1 . Banda imara ni rafiki kwake 
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe 
3 Mchaganyo bora wa chakula 
4. Tiba bora na kinga 
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake ) 

CHANGAMOTO 

KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA. 
Katika ufugaji wa nguruwe kuna chagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama: 
Matatizo ya kupumua 
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatega au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto. 

Baridi 
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga. 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabada ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi. 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga 
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga: 
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa. 
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto. 
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatubaada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu. 
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya. 
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe. 
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao 
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa. 
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo 
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka. 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya 
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza. 
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana. 
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu. 
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na 
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE 
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara. 
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia. 

JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50 
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) . 
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu 
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora. 
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/= 
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/= 
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/= 
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/= 
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/= 
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/= 
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000 
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/= 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA . 
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia 
MAANDALIZI YA CHAKULA 
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA 
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili. 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5 
N:B ikumbukwe hapo nyuma nilitoa mchaganuo wa nguruwe 40 ndiyo maana makandilio yalikuwa kwenye million 3.5 ama 3 kamili. 
KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE 
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane . 
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika 
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50. Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili. 
Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ? 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO. 
chukua kalamu na karatasi fanya hesabu mwenyewe kwa mtaji wako na namna unavyoweza usipopata faida nipigie simu pia ukipata faida nipigie simu kwa maelezo zaidi na msaada zaidi 
POINT TO NOTE, pia kwa wale wanaohitaji kufanya hii project hawana eneo wala uhakika wa chakula na lishe na usimamizi thabiti wa kitaalamu na wenye tija. tuwasiliane Kwa msaada zaidi. 

NYOGEZA 
Nguruwe 20 wanaweza kukugharimu million mbili unapoanzisha mradi na kukupa faida isiyopungua million 20 kwa uzao wa kwanza na uzao wa pili utapata uhakika wa jumla ya million 40 ukitoa gharama zote hazitozidi milio 5.5 
Nguruwe 10 wanaweza kukugharimu million moja na point unapoanzisha mradi na kukupa faida na kukupa faida ya million 10 kwa uzao wa kwanza ukijumlisha na uzao wa pili utapata uhakika wa kuwa na million 20 ukitoa gharama zote hazitozidi million 4.5 
Nguruwe 5 wanaweza kukugharimu laki tano na point unapoanzisha mradi na watakupa faida ya zaidi ya million5 kwa uzao wa kwanza na uzao wa pili watakupa jumla ya million 10 ukitoa gharama zote hazitozidi million 3 
Kumbuka hesabu zangu zote nimeweka kwa makadirio ya juu hivyo ukienda kwenye uhalisia nakufata kanuni za ujasirimali lazima zipugue asilimia 5 au 10 ya jumla yote niliyotoa
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Share Now

Related posts