UGONJWA WA MAFUA YA KUKU I Mshindo Media (new)

#UFAHAMU UGONJWA WA MAFUA YA KUKU

Ni ugonjwa unaoitwa infectious coryza huenezwa na

bacteria. anaeitwa (hemophilus paragallinarum).

Ugonjwa huu hushambulia kuku aina zote. Na usipo kuwa

makini kwenye usafi wa banda na vyombo , kuruhusu watu kuingia ovyo bandani au kuku wa jirani kuja kuingia

kwenye banda lako; ugonjwa huu unaweza shambulia kuku wako kwa kila wiki.

#DALILI ZA UGONJWA HUU

_Kuvimba uso chini na nyuma ya macho.

_Kupumua kwa shida na kukoroma

_Kutoka makamasi puani,

_ Mdomoni kuwa na hali ya mterezo

_Macho kuvimba

_Kushindwa kula.

_Kupiga chafya , macho kuonekana kama yanatoka

machozi

#JINSI UGONJWA UNAVYOENEA

_Ugonjwa huu huenea kutokana kuku mmoja kwenda kwa

kuku mwingine, au kutoka banda moja kwenda banda

lingine.

_Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilicho

chafuliwa na kinyesi cha kuku Mgonjwa.

_Ugonjwa huu uneea na kuambukizwa kwa mfumo wa

hewa pale kuku wanapopiga chafya.

#UNASHAURIWA

Pindi ugonjwa unapo ingia bandani kwako wale kuku

watakao onesha dalili za ugonjwa huu , watenge kisha

wape tiba kuku wako wote; unatakiwa kuwatenga kwa ajili

ya kupunguza maambukizi bandani.

#DALILI ZA MZOGA UKIUPASUA

Usaha mweupe hadi njano huonekana kwenye macho na

ndani ya pua

#MATIBABU

Zipo dawa nyingi za kutibu ugonjwa huu antibiotic/ sulfa.

Hizi ni baadhi tu.

Fluban

Flutan

Ganadexil

Tylodox

Teramycin.

Trimazine nk

#Ushauri:

Tumia fluban,flutan kwa Kuku wanaooneshadalili za mafua bila vifo.

Tumia Ganadexil,tylodox kwa Kuku wenye mafua ambao

kuna vifo vingi

…………………………………………………………………………………………………………………………….

Share Now

Related posts