RATIBA ZA CHANJO KWA KUKU TOKA VIFARANGA (new) I Mshindo Media

https://www.mshindoveterinarycentre.com/ RATIBA ZA UTOAJI CHANJO

Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:

1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:

Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,

Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,

Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.

2. Umri wa kuchanja kuku:

Kwa kuku ambao wanatarajiwa kutaga mayai au kuwa kuku wazazi, chanjo

nyingi hutolewa si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuku kuanza kutaga. Pia kuna baadhi ya chanjo ambazo haziruhusiwi kwa kuku wadogo. (Angalia Ratiba).

3. Magonjwa muhimu katika eneo husika:

Ni muhimu sana kuelewa magonjwa ya kuku yaliyopo katika eneo lako kabla ya kuandaa programu ya uchanjaji, hasa kwa yale magonjwa ambayo chanjo zenye

Vimelea hai hutumika. Hivyo basi, sio busara kuanza kutumia chanjo za aina hii katika maeneo ambayo

Ugonjwa huo haujawahi kuripotiwa.

4. Hali ya kiafya ya kuku watakaochanjwa:

Usiwape chanjo kuku ambao wanaonyesha dalili za kuathirika kwa mfumo wa hewa au wanaonyesha kuwa na minyoo au wadudu wengine. Kwa kuku walio na dalili hizi chanjo zinaweza kuleta madhara na zisifanye kazi.

5. Aina ya kuku watakaochanjwa:

Kuku wanaofugwa kwa ajili ya nyama wanahitaji kinga ya muda mfupi, hivyo basi chanjo moja inaweza kutosha kabla ya kufikia umri wa kuuzwa. Lakini kuku wa mayai na kuku wazazi wanahitaji programu ya chanjo ambayo itawakinga na magonjwa kwa kipindi chote wanapokua na kutaga. (Zingatia Ratiba).

6. Historia ya Magonjwa katika shamba:

Kabla ya kuandaa mpango wa chanjo, lazima ufahamu ni

Magonjwa gani yaliyoenea katika shamba.

a) Kama unataka kuingiza kuku wapya kutoka mahali ambako ugonjwa umeshawahi kutokea,

kuku hao wachanjwe wiki 3 kabla ya kuwaingiza shambani

b) Iwapo utatumia chanjo yenye vimelea hai, hakikisha kwamba magonjwa hayo yameshawahi

kutokea katika shamba husika. Usitumie chanjo hizi katika shamba ambalo ugonjwa huo

haujawahi kutokea au kutambuliwa.

c) Wasiliana na mashamba jirani kufahamu iwapo wanatumia chanjo zenye vimelea hai. Toa taarifa

kwa mamlaka za mifugo iwapo unapanga kutumia chanjo hizo katika eneo lako. Pata ushauri wa daktari.

TARATIBU ZA UCHANJAJI

Mambo muhimu ya kuzingatia:

•Hakikisha unazingatia kwa makini masharti ya mtengenezaji wa chanjo: jinsi ya kuhifadhi, kutayarisha na njia inayotumika kumchanja kuku. Wakati wote zingatia masharti ya mtengenezaji kuhusu uhifadhi wa

chanjo ili isipoteze nguvu.

• Fuata ushauri wa daktari wa mifugo unapoandaa programu ya chanjo.

• Watoa chanjo wapatiwe mafunzo ya jinsi ya kutayarisha na kutoa chanjo

• Chagua aina ya chanjo kulingana na umri na hali ya kiafya ya kuku.

• Fanya usafi wa mara kwa mara katika mabanda ili kupunguza wingi wa vimelea kwenye mazingira.

• Tumia maji ambayo hayajawekwa dawa au kemikali kwa ajili ya kuchanganyia chanjo, k.m. maji ya kisima, mvua, n.k. Maji ya kuchanganyia chanjo yawe na ubaridi, yasiwe moto.

• Changanya chanjo kabla ya kutumia na iwekwe mbali na kuku.

• Pata ushauri wa daktari wa mifugo kabla ya kuchanja kuku wagonjwa au wale ambao hawako katika

muonekano mzuri

• Siku ya chanjo, usiwape kuku maji kwa masaa 3 – 4 ili waweze kunywa maji yaliyowekwa chanjo kwa

haraka.

• Zoezi la uchanjaji lifanyike haraka ili kupunguza usumbufu kwa kuku.

• Tenganisha kuku waliochanjwa na wale ambao hawajachanjwa.

• Baada ya kuchanjwa, kuku wawekwe kwenye banda linalopitisha hewa vizuri

• Baada ya kila zoezi la kuchanja, wafanyakazi wabadilishe mavazi, viatu/buti zisafishwe na kuwekwa dawa, na vifaa vilivyotumika viwekwe dawa ya kuua vimelea.

• Fuata utaratibu uliowekwa wa kuharibu/kusafisha vifaa vilivyotumika kuchanja

• Weka kumbukumbu za uchanjaji vizuri

Mambo ambayo hutakiwi kuyafanya unapochanja

• Kumwaga chanjo ovyo na kuchafua mikono au nguo

• Kuchanganya chanjo za aina mbili au zaidi, isipokuwa pale tu mtengenezaji wa chanjo atakavyoagiza

hivyo, au kwa ushauri wa daktari wa mifugo.

• Kutumia chanjo iliyopita muda wake

• Kutumia chanjo iliyobaki ili itumike kwa kazi ya siku nyingine

• Kuchanja kuku ambao wamepatiwa dawa aina ya antibiotiki.

• Kuchanja zaidi ya chanjo moja kwa wakati, iwapo haikuagizwa hivyo.

CHANJO ZINAZO PENDEKEZWA

Aina ya Chanjo

Umri wa Kuchanja Kuku

Muda kati ya kutoa chanjo

Njia inayotumika kuchanja kuku

Lasota – kwa ajili ya Mdondo/Kideri

Kifaranga wa Siku 3

Rudia baada ya siku 21, baada ya hapo kila baada ya miezi 3

Maji safi yasiyowekwa dawa

Chanjo inayohimili joto – I-2 kwa ajili ya Mdondo/Kideri

Kifaranga wa Siku moja

Rudia baada ya kila miezi 4 kwa kuku wa mayai na wazazi

Tone la chanjo kwenye jicho kwa kila kuku

Hipraviar-B1 – kwa ajili ya

Mdondo/Kideri na Ugonjwa wa Mapafu (Infectious Bronchitis)

Kifaranga wa Siku moja

Rudia baada ya siku 21, baada ya hapo kila baada ya miezi 3

Maji safi yasiyowekwa dawa

VIR-114 – kwa ajili ya Gumboro

Siku 10 au 14

Inaweza kurudiwa Siku ya 17 kwa

wale waliochanjwa wakiwa na Siku

10; na Siku ya 28 kwa wale waliochanjwa wakiwa na Siku 14

Maji safi yasiyowekwa dawa.

Avipro – kwa ajili ya Ndui ya Kuku

Wiki 7 hadi 14

Chanjo moja Chanja katikati ya ngozi

kwa kutumia utando wa ngozi kwenye bawa

Chanjo ya Mareksi

Kifaranga wa Siku moja

Chanjo moja

………………………………………………………………………………….

Share Now

Related posts