Njia tofauti za kufuga kuku. Faida Na Hasara Zake (new) I Mshindo Media

Mambo yanayomfanya mfugaji kuamua atumie njia fulani ya kufuga ni pamoja na uwezo wa  kugharamia shughuli ya ufugaji wa kuku na ukubwa wa eneo alilonalo la kufugia. Katika sehemu hii utajifunza njia tatu za kufuga kuku ambazo ni:  1. Kufuga huria Kuku huachwa wenyewe kujitafutia chakula na maji. Njia hii inatumika zaidi kufuga kuku wa kienyeji. Mara chache sana mfugaji huwapatia kuku chakula cha ziada. Kwa ufugaji huu lazima kuwe na eneo kubwa la kutosha kuku kuzunguka na kutafuta chakula. Kuku hulala eneo lisilo rasmi kama vile jikoni, kwenye kiambata n.k.…

JINSI YA KULEA VIFARANGA (new) I Mshindo Media

SOMO:KULEA VIFARANGAUnayapata hapa kupitia Website yako pendwa Hapa SEHEMU YA 1: BANDA BORA LA VIFARANGA Habari ya uzima ndugu mfugaji! Huu ni mwanzo wa somo la kulea vifaranga , tutajifunza ujenzi wa banda la vifaranga, vitu vya muhimu katika banda la vifaranga, kujiandaa kupokea vifaranga, chanjo na dawa, sababu za vifo kwa vifaranga , lishe bora kwa vifaranga, na jinsi ya kudhibiti vifo nk. Mwanzo huu ,sehemu ya kwanza tutajifunza ujenzi wa banda la vifaranga/ vitu vya muhimu katika banda la vifarangaï‘Š. ï‘ŠNyumba Ya Kulelea Vifarangaï‘Š Ukipenda kujenga nyumba ya vifaranga itafaa ujue …

ULEAJI WA VIFARANGA WA KIENYEJI KWA NJIA YA KISASA (new)

UFUGAJI WA KUKU JINSI YA KUTUNZA VIFARANGA WIKI 1-5 Kuku ni ndege wafugwao na binadamu wengi kwa ajiliya matumizi mbalaimbali ya binadamu. Mara nyingi hutumika kwa ajili ya kitoweo na kwa biashara pia. Wafugaji wengi hupenda kufuga kuku maana ni mwepesi kumtunza na hana garama kubwa za utunzaji ukilinganisha na wanyama wengine wafugwao. leo tutaangali jinsi ya kuwalea vifaranga had wafae kuwa kuku wakubwa; Nyumba ya vifaranga; nyumba ya vifaranga inatakiwa kuwa karibu na nyumba ya kuishi ili uweze kuwaangalia vifaranga kwa ukaribu zaidi, ijengwe kwenye sehemu iliyotulia kulingana na…

Ufugaji Bora wa Kuku wa Kienyeji/asili (new)

KUKU WA ASILI Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya.  Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.  Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali.  Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa…

MUHTASARI WA UFUGAJI KUKU I Mshindo Media (new)

1: Maandalizi ya banda la kuku, Fagia, deki kwa maji, pulizia dawa/disinfection (Th4, V rid,Farm guard nk).  Acha banda likae zaidi ya siku 7 baada ya kutoa kuku wakubwa kabla ya kuingiza kuku wengine.  Andaa vifaa vyote muhimu kwa ajili ya kupokea kuku wapya vikae bandani angalau siku 3 kabla ya kupokea vifaranga. Andaa sehemu ya kulelea vifaranga, weka vyanzo vya joto tayari kabla vifaranga hawajafika(Usikurupuke kuweka wakati vifaranga wameshafika).  2: Maandalizi ya chakula na maji  Hakikisha maji, chakula kwaajili ya kuku wako yapo bandani au sehemu ya karibu muda…

ZINGATIA HAYA KABLA YA KUANZA MRADI WA UFUGAJI WA KUKU (new) I Mshindo Media

1.Zingatia kanuni na USHAURI bora juu ya ufugaji wako 2.Chagua mbegu bora ya kuku inayoendana na soko lako  3.Fikiria njia za kutatua CHANGAMOTO ulizozibaini katika UFUGAJI 4.Fanya uchunguzi wa soko la kuku wako kabla ya kuagiza  5.Piga hesabu ya UWEKEZAJI wako wa mradi kuanzia mwanzo hadi mwisho  6.Hakikisha umepata maelekezo sahii juu ya ufugaji kabla ya kuanza kufuga Chakula Cha Kuku Kuna vitu vitano muhimu vinavyotaijika kwa kuku ili awe na afya bora. Navyo ni kama vifuatavyo, 1. PROTININi aina ya vyakula ambavyo kazi yake kubwa ni kukuza mwili navyo ni kama…

MBINU KUMI ZA KUFUGA KUKU KWA MATOKEO BORA ZAIDI (new) I Mshindo Media

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala zetu na mfugaji wa kuku.Ni imani yetu kuwa uko sawa kabisa na mradi wako unaenda kama ulivyotegemea.Kama mambo hayaendi sawa basi endelea kuwasiliana nasi tusaidiane kukabiliana na changamoto unazopitia na kushauriana zaidi.Leo tungependa kutoa elimu mujarabu juu mbinu  sahihi za kufuga kuku ili mfugaji aweze kupata matokeo mazuri katika ufugaji wake. 1. Mtaji; Kabla hujaamua aina ya kuku wa kufuga ni vema ukabaini hali yako kifedha. Maana kuku hutofautiana katika ufugaji kwa gharama zao. Hivyo ni lazima ukajua kiasi ulichonacho kulingana na kuku…