Jinsi ya kulea vifaranga/kuku wa kienyeji (new) I Mshindo Media

MAFUNZO MBALI MBALI RAHISI NA HALISI KWA MFUGAJI 

ULISHAJI 
👉Lisha kuku muda mmoja kila siku, usibadilishe badilishe ratiba 
👉Usibadilishe badilishe chakula 
👉Usiwapunje wala kuzidisha chakula 
👉Wawekee vyombo vya kutosha 
👉Maji yawepo muda wote 
👉Vyombo vya maji visafishwe kila siku 

 UOKOTAJI WA MAYAI 
 👉Panga ratiba maalumu ya kuokota mayai, mfn SAA 7:30/Am, saa 10:30 Am, saa 1:30 Pm, saa 4:30 Pm, funga report. 
👉Safisha viota vya kuku, kuondoa vinyesi kila asubuhi na ongeza matandazo mayai yasipasuke 
👉Okota mayai na yaweke kwenye Trey upande uliochongoka utazame chini, na upande butu uwe juu 
👉Weka mayai sehemu salama isiyo na joto jingi 
👉Mayai ya kutotolesha yahifadhiwe kwa siku zisizo zidi 10 

 UHIFADHI WA KUMBUKUMBU 
👉Hakikisha umeweka kumbukumbu zote za msingi shambani kwako kama 
👆Aina ya kuku 
👉Siku ya kuingia bandani 
👉Idadi yao na wanaokufa 
👉Gharama za chakula 
👉Gharama nyingine zote 
👉Mauzo 
🐣Piga hesabu mapato na matumizi, hii itakusaidia kujua na kutathmini kama mtaji unakupa faida au unajiendesha kwa hasara. 

 BIOSECURITY/VIUMBE HAI SALAMA 
👉Usichanganye kuku na mifugo wengine 
👉Usiruhusu kila mtu kuingia bandani 
👉Mavazi maalumu na buti maalumu za bandani 
👉Panya na ndege wazuiwe kuingia bandani uwezavyo 
👉Kuku wachanjwe kwa wakati 
👉Kuku waliokufa waondolewe bandani kwa wakati 

JIONGEZE KITAALUMA 
👉Wapeleke watunzaji kuku semina za ufugaji 
👉Kama mmiliki hudhuria warsha na maonesho kujifunza ufugaji 
👉Uwe mfuatiliaji wa mradi wako Mara kwa Mara 
👉Ajiri /tafuta mtaalamu kuwa anaangalia mradi wako 
👉Lipa vizuri wafanyakazi wako🐣 

UPANUZI WA MRADI 
👉Tafuta wateja wapya kila wiki 
👉Imarisha uaminifu kwa wateja wazamani 
👉Hakikisha bidhaa haiishi bandani, kama itaisha tafuta namna ya kumuwezesha mteja kupata bidhaa , ukikosea wanakimbia. 
👉Panua mradi pindi gharama za uanzishaji zinapo rejea, usisubirie mpaka kuku wazeeke 

MUHIMU 
👉Ukihitaji uzalishaji bora usiogope kugharamia wataalamu 
👉Pata miongozo tofauti ya ufugaji kupanua uelewa 

Share Now

Related posts