JIFUNZE UGONJWA WA NDUI YA KUKU NA TIBA YAKE (new) I Mshindo Media

NAMNA YA KUTIBU UGONJWA WA NDUI YA KUKU KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI. DALILI ZA UGONJWA WA NDUI.· Ugonjwa wa ndui utaona kuku wako wamepata mapele kwenye kichwa yenye rangi ya kahawia, mapele hayo yanaweza kuziba mpaka macho kufanya kuku wako wasione kabisa na kusababisha kuku wako wakashindwa kula hivyo wakadhoofika kabisa na hatimaye kufa. Ugonjwa huu huwapata kuku wa rika zote lakini huathiri sana vifaranga. Mara nyingi magonjwa ya virusi ni magonjwa ambayo hayana tiba lakini yana kinga. Wape chanjo kuku wako hasa vifaranga wanapokua wamefikia umri wa siku…

VIOTA VYA KUKU /chicken nest (new) I Mshindo Media

Kiota ni sehemu ambayo kuku utaga mayai , kuatamia na kutotoa VIFARANGA Aina za viota (type of nest) 1.Kiota kilichotengenezwa na kuku mwenyewe  Ambapo kuku mwenyewe uchagua mahali pa kutagia na kuhifadhi mayai2.Kiota kilichoandaliwa na MFUGAJI Aina ya viota hivi uandaliwa na MFUGAJI katika njia stahiki ili kuweza kupata mazao imara MAHITAJI  YA MUHIMU KATIKA KIOTA Boksi la karatasi Mbao  Nyasi  Nguo ya Aina pamba Ukubwa wa KIOTA inatakiwa uwe unamwezesha kukaa na kujigeuza  Hii maana yake ni inatakiwa uwe na sentimita 35 upana sentimita 35 na urefu sentimita 35…

JINSI YA KUCHAGUA MATETEA YANAYOWEZA KUATAMIA MAYAI (new) I Mshindo Media

Yaweza kutokea baadhi ya kuku wakawa watagaji wazuri wa mayai lakini hawapendi kuatamia. Katika hali hiyo ni vyema wakachaguliwa kuku (mitetea) wengine ili kuatamia mayai yao kwa uanguaji mzuri. UTARATIBU UFUATAO UTATUMIKA Tafuta mtetea aliyefikia umri wa kutaga au kuku aliyekwishawahi kutotoa. Tafuta mawe matatu ya mviringo au viazi mbatata vya ukubwa wa yai au vibao vilivyochongwa kwa umbile la yai au mayai yasiyo na mbegu (mayai viza, au ya kuku wa kisasa). Muwekee kuku huyo mayai bandia yasiyopungua matatu kwenye kiota wakati wa usiku na umfungie humo usiku kucha…