CHAKULA CHA KUKU WA KIENYEJI/CHOTARA (new) I Mshindo Media


JINSI YA KUCHANGANYA CHAKULA CHA VIFALANGA  WA KIENYEJI 

MIEZI MIWILI YA MWANZO

Unga wa dona wa nafaka kama mahindi au mtama 40kg
Pumba za mtama au mahindi au uwele 27kg
Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 20kg
Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25kg
Dagaa au mabaki ya samaki (sangara fish meal) 10kg
Chumvi ya jikoni 0.5
Virutubisho (Broiler premix) 0.25
JUMLA = 100kgs.

Huu mchanganyiko ni wa vifaranga kuanzia siku 1 hadi miezi miwili.

NJINSI YA KUCHANGANYA CHAKULA CHA KUKU WA KIENYEJI, . WA  MIEZI 3 MPAKA WA 4.

Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 25
Pumba za mtama au mahindi au uwele 44
Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 17
Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 3.25
Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 10
Chumvi ya jikoni 0.25
Virutubisho (Broiler premix) 0.5.
JUMLA = 100Kgs

NJINSI YA KUCHANGANYA CHAKULA CHA KUKU WA KIENYEJI,. WA  MIEZI 5 MPAKA WA 6. (Hadi kuuzwa)

Mahindi yaliyobarazwa au mtama au uwele 31
Pumba za mtama au mahindi au uwele 38
Mashudu ya alizeti au ufuta, au pamba au karanga n.k. 18
Unga wa mifupa au chokaa ya kuku (DCP) 2.25
Dagaa au mabaki ya samaki (fish meal) 13
Chumvi ya jikoni 0.5
Virutubisho (Broiler premix) 0.25
JUMLA = 100 kgs

Nb mchanganyiko huu ni kwa ajili ya kuku wa biashara hu mfanya kuku awe na mafuta. Ila kama kuku wako unataka badae waje watage katika mchanganyiko huo utawapa mwisho kwenye mwezi wa Tatu.
Kuanzia mwezi wa nne utawapa mchanganyiko huu hapa chini ili kuwa andaa kwa ajili ya kutaga

KWA KUKU KIENYEJI WANAO TAGA.

Dagaa  2 kg
Damu   2 kg
Alizeti    8 kg
Pumba ya mahindi   5 kg
Mahindi yalio barazwa    24 kg
Chokaa    5 kg
Mifupa    4 kg
Layers premix gm  150
Methionine gm  50
Chumvi  gm 30

…………………………………………………………………………………………………………………

Share Now

Related posts